Mkurugenzi wa kampuni ya msama promotion bw. Alex Msama , akiwaonesha waandishi wa habari hawapo pichani baadhi ya Computer zilizokamatwa pamoja na wanaozilimiliki na kufanya kazi haramu ya kudurufu kazi za wasanii, jumla ya computer zenye thamani ya milioni 47 zilisamilishwa kituo kikuu cha polisi mjini Dodoma.(PICHA ZOTE NA DIRA MEDIA).
Askari wa kituo kikuu cha polisi mjini Dodoma akisaidia kuziweka pamoja moja ya Computer zenye kudurufu kazi za wasanii kwa njia haramu , wakati wa msako wa kukamata wezi wa kazi za wasani ulioendeshwa na Kampuni ya Msama Promotion mjini humo, wanao onekana pichani ni baadhi ya watuhumiwa waliokamatwa na kufikishwa kituoni hapo.